• Biashara Bora

    0

    Zaidi ya asilimia 80 ya biashara mpya hufa kabla ya kutimiza miaka miwili. Hapa utajifunza aina za biashara bora, mambo ya kuzingatia kabla ya kuanzisha biashara, sifa na tabia za biashara bora ili uanzishe, uzalishe, umiliki na uwekeze katika biashara.

    Sh15,000.00
    Add to cart
  • Ongeza Kipato Chako

    0

    Kama unatamani kuongeza kipato chako kwa sasa na kuwa na uhakika wa kuendelea kuwa na kipato kinachojitosheleza hadi pale utakapozeeka na uache urithi mzuri kwa kizazi chako kinachofuata, kitabu hiki kitakufaa sana kwa sababu utapata ufahamu sahihi juu ya fedha, uwekezaji na biashara na katika namna unayoweza kufanyia kazi kuanzia leo. Utajifunza jinsi ya kupanga bajeti yako ili upate ziada ya akiba na uwekezaji, pia kutengeneza mkakati wa muda mrefu wa kupata uhuru wa kifedha.

    Sh15,000.00
    Add to cart
  • Timiza Malengo Yako

    1

    Je una malengo ya kufanikiwa katika maisha yako? Kitabu hiki kinatoa mbinu ambazo wengi wamezitumia na wanaendelea kuzitumia duniani kote ili kufikia malengo waliyojiwekea katika maisha yao. Ukweli ni kuwa watu hawashindwi kutimiza malengo yao kwa sababu hawana uwezo na shauku ya kufanya hivyo, bali kwa sababu wameshindwa kujua wafanye nini ili kutimiza malengo waliyonayo katika maisha yao. Katika kitabu hiki utajifunza mambo kadhaa ikiwemo namna ya kuweka malengo yanayofanikiwa. kujua kusudi lililofanya uzaliwe. Mbinu za kuifanya ndoto yako kuwa uhalisia

    Sh20,000.00
    Add to cart
  • Saikolojia ya Mteja

    0

    Katika Biashara yoyote ambayo mtu anaifanya awe anatoa huduma au anauza bidhaa, moja ya uwezo mkubwa sana anatakiwa kuwa nao ni uwezo wa kuhudumia wateja. Na hii imekua ni changamoto kwa watu wengi. Kitabu hiki kimeandaliwa maalumu kwa ajili ya kukupatia maarifa sahihi juu ya saikolojia ya mteja na utajifunza mambo mengi yatakayobadilisha ufahamu wako juu ya mteja.

    Sh15,000.00
    Add to cart
  • Hazina ya Penzi

    0

    Kuna watu ambao huamini hakuna mapenzi ya kweli duniani, na kuna wanaokubali mapenzi ya kweli yapo. Na hawa wotewanaongea kutoka katika maisha ambayo wameishi, mazingira wakiyokulia, mambo waliyoshuhudia, waliyosoma na pengine waliyofanyiwa. Pamoja na yote hayo bado haiondoi ukweli kwamba mapenzi imekuwa mada na swala linaongelewa sana Ulimwenguni kote. Watu wameua kwa sababu ya mapenzi, watu wameumwa, wamejeruhi, wamejenga uadui kwa sababu ya jambo hili mapenzi.

    Sh15,000.00
    Add to cart
  • Malezi Yenye Tija

    0

    Jamii ya sasa ina changamoto nyingi na nyingine hazikwepeki, yapo maendeleo ya kiteknolojia, kiviwanda, kiuchumi na kijamii. Maendeleo haya tukubali au tusikubali yanaathiri eneo la familia na malezi kwa kiasi kikubwa sana. Leo tunashuhudia ongezeko kubwa sana la wazazi wanaolea watoto bila mzazi mwenza. Changamoto hii imenifanya kuandika kitabu hiki ili kumsaidia mzazi, mlezi na yeyote mwenye mawazo ya kuja kuwa na familia huko mbeleni ili kuweza kupata ujuzi na uelewa wa mambo ya ndani kabisa yahusuyo malezi ya watoto wetu. Hakuna aliyezaliwa na ujuzi mkubwa wa malezi. Tunajifunza na tunafundishana. Nikutakie wakati mwema na akili iliyotulia katika kusoma na kukifurahia kitabu hiki. Kusoma tu hakutokusaidia sana. Msaada na manufaa makubwa utayapata pale ambapo utaamua kukiweka kitabu hiki katika matendo.

    Sh15,000.00
    Add to cart
  • Mpe Mungu Ibada Kamili

    0

    In this book you will learn how to offer spiritual sacrifices acceptable to God through Jesus Christ, which are your body, praise, thanksgiving, prayer, offering and service to God. God desires for us to give him our total worship and not partial worship. As a believer you have been made a priest for the purpose of offering all spiritual sacrifices unto God. This is a call to a spiritually balanced life where worshipping God becomes the way of life.

    Sh20,000.00
    Add to cart